Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 87 2021-11-11

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha uwepo wa marubani wawili kwenye ndege ndogo za abiria?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Khalifa Mohamed Issa, Mbunge wa Mtambwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ndege zote kwa mujibu wa vyeti vya utengenezaji (type certificate) huwa zina taarifa inayoelekeza mambo muhimu ya kifundi na usalama yahusuyo operesheni za ndege hizo. Pamoja na hizo nyaraka mbili, pia kuna kitabu cha maelekezo ya matumizi. Ndege zote zenye uzito wa kilogramu 5,700 kwenda chini ni ndege za rubani mmoja kwa mujibu wa nyaraka za mtengenezaji.

Mheshimiwa Spika, aidha, kwa mujibu wa Sheria ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga na Sheria ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga, haizuii ndege hizo kuendeshwa na rubani mmoja na ni salama kufanya hivyo. Hata hivyo, nchi yetu imeweka sheria ya kuwa na marubani wawili kwa ndege yoyote ya abiria yenye uzito unaozidi kilogram 5,700 hata kama mtengenezaji wake anaruhusu rubani mmoja mmoja, katika kujiwekea wigo mpana wa kuweka usalama wa anga.

Mheshimiwa Spika, aidha, Mamlaka ya Usafiri wa Anga imeweka utaratibu wa kuhakiki afya za marubani mara kwa mara kwa mujibu wa sheria. Uhakiki wa kati na mkubwa hufanyika kila baada ya miezi sita kwa marubani wenye umri unaozidi miaka 40 na kila baada ya miezi 12 kwa marubani wenye umri wa chini ya miaka 40. Uhakiki wa mara kwa mara na wa kushtukiza pia hufanyika. Aidha, rubani yeyote anayekutwa na changamoto za kiafya huwekewa sharti la kutoruka peke yake au kuzuiwa kuruka kabisa. Ahsante.