Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 85 2021-11-11

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kuendeleza Mradi wa Maji wa Lukululu ili kumaliza tatizo la maji katika vijiji 14 vya Jimbo la Vwawa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji wa Lukululu unatekelezwa kwa awamu ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kujenga miradi ya maji katika vijiji vitano kati ya 15 vya Mradi wa Maji Lukululu ambavyo ni Myovizi, Mbewe, Mahenje, Mlangali na Ndolezi. Kazi zitakazofanyika ni ujenzi wa matanki manne ambapo kwa pamoja yatahifadhi maji lita 450,000 na mtandao wa mabomba wa urefu wa kilomita 58.3. Kazi hii itaanza kutekelezwa mwezi Desemba, 2021.

Mheshimiwa Spika, awamu ya pili itahusisha Vijiji 10 ambavyo ni Mbulu, Ivugula, Igunda, Ichesa, Shaji, Shomola, Shidunda, Ilea, Mbwewe na Lukululu. Kazi ya usanifu imepangwa kukamilika robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2021/2022 na matarajio ni kupatikana Mkandarasi na utekelezaji utaanza Julai, 2022.

Mheshimiwa Spika, jitihada hizi za Serikali zinalenga kuboresha huduma ya upatikanaji majisafi na salama Wilayani Mbozi.