Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 83 2021-11-11

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani ya kupunguza au kuondosha kabisa wizi wa mazao ya kilimo na mifugo katika maeneo ya Unguja na Pemba?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge wa Donge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi nchini ndilo lenye jukumu la kulinda maisha na mali za wananchi na linatambua suala la uhalifu na wizi wa mifugo na wizi wa mazao ya kilimo unaosumbua wananchi wa Zanzibar, katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Septemba 2021 jumla ya matukio 72 ya wizi wa mifugo na 85 ya wizi wa mazao umeripotiwa katika vituo vya Polisi. Watuhumiwa 48 wa wizi wa mifugo na 52 wa wizi mazao wamekamatwa na kesi 22 za wizi wa mifugo na 36 za wizi wa mazao zinaendelea mahakamani na ziko kwenye hatua mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi kuanzisha na kushiriki kwenye vikundi vya ulinzi shirikishi ili kuzuia uhalifu na Jeshi la Polisi litaendelea kufanya doria kwenye maeneo yote ili kudhibiti na kutokomeza uhalifu hapa nchini. Nakushukuru.