Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 56 2021-11-08

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa Vituo vya Polisi vilivyopo katika Kata za Kilema, Kirua Vunjo, Kahe na Marangu katika Jimbo la Vunjo vinapewa usafiri?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uhitaji mkubwa wa magari katika vituo vya Polisi vilivyo katika Jimbo la Vunjo ambavyo ni Kilema, Kiruavunjo, Kahe na Marangu kama vyanzo muhimu katika kutendea kazi. Kwa kupitia mkataba wake wa kampuni ya Ashok Leyland ya nchini India, Jeshi la Polisi linategemea kupokea magari 369 na pindi magari hayo yatakapofika kipaumbele kitatolewa kwa vituo vya polisi vyenye uhitaji mkubwa ikiwemo kituo ama vituo vilivyo katika Jimbo la Vunjo. Nakushukuru.