Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 52 2021-11-08

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: -

Barabara ya Mlimani kutoka Mwembe – Mbaga hadi Mamba - Myamba ni kero kubwa kwa wakazi zaidi ya 150,000 katika Majimbo ya manne; Same Magharibi na Same Mashariki ambapo zaidi ya 70% ya wakazi wake wanaishi milimani.

Je, ni lini barabara hiyo yenye urefu wa Km 120 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami nyepesi (Surface dressing) ili kufanikisha shughuli za maendeleo katika Wilaya ya Same?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mwembe – Myamba hadi Ndungu ni barabara ya changarawe yenye urefu wa kilometa 90.19. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Aidha, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/ 2022, Serikali imetenga shilingi milioni 1,848.97 kwa ajili ya kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hiyo. Vilevile, ujenzi wa Daraja la Yongoma lililokatika wakati wa msimu wa mvua umekamilika kwa gharama ya shilingi milioni 453. Ahsante. (Makofi)