Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 45 2021-11-05

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO K.n.y. MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro uliopo katika eneo lenye madini ya Jasi kati ya Wananchi wa Kata ya Bendera Mkoani Kilimanjaro na Wananchi wa Kata ya Mkomazi Mkoani Tanga?

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini, imetoa leseni za uchimbaji mdogo katika maeneo hayo ya Kata ya Bendera iliyopo Mkoani Kilimanjaro na Kata ya Mkomazi iliyopo Mkoani Tanga.

Mheshimiwa Spika, katika maeneo hayo ya kata hizo mbili, hivi tunavyoongea, hakuna mgogoro wowote unaohusiana na leseni za uchimbaji mdogo wa madini ya Jasi na wachimbaji wanaendelea na shughuli zao kama kawaida. Nakushukuru. (Makofi)