Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 39 2021-11-05

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO S. GAMBO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Wenyeviti wa Serikali za Mitaa wanapata malipo kama Madiwani na Wabunge kutokana na majukumu mazito wanayoyafanya ikiwemo ufuatiliaji wa malipo ya Kodi ya Majengo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua na kuthamini kazi kubwa inayofanywa na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji kwa kuwa ndio wasimamizi wakuu wa shughuli zote za maendeleo katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ngazi ya Vijiji na Mitaa za Mwaka 2014 chini ya Tangazo la Serikali Na. 322, miongoni mwa sifa zinazomwezesha mkazi wa Kijiji, Mtaa au Kitongoji kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti ni pamoja na kuwa na shughuli halali inayomwingizia kipato.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilitoa mwongozo kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhusu malipo ya posho ya viongozi hawa kwa kutumia mapato ya ndani kadri ya uwezo wa Halmashauri. Kwa ujumla, uwezo wa Halmashauri zilizo nyingi bado ni mdogo katika kutekeleza jukumu hili. Hivyo, Serikali imeichukua changamoto hii na itaendelea kufanya tathmini. Ahsante.