Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 37 2021-11-04

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kuwajumuisha Wenyeviti wa Halmashauri na Wabunge kwenye Kamati za kujadili na kupitisha maombi ya wavunaji wa mali za misitu kwenye Wilaya zetu nchini?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi, uwakilishi wa wananchi upo katika ngazi mbili. Ngazi ya kwanza ni ambapo Wenyeviti na Watendaji wa Vijiji vinavyovuna hushiriki kwenye vikao vya Kamati, ngazi ya pili ni ambapo Waheshimiwa Madiwani na Wabunge katika vikao vya Baraza la Madiwani hupata wasaa wa kujadili na kutoa ushauri juu ya taarifa za Kamati zinazohusu maombi yote ya uvunaji wa miti na tathmini ya mwenendo wa uvunaji katika Wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, ugawaji wa malighafi ya miti ya kuvunwa katika misitu ya asili ya Serikali unasimamiwa na Kamati ya Usimamizi ya Uvunaji katika kila Wilaya. Jukumu la kwanza la Kamati hii ni kujadili na kutoa maamuzi ya maombi ya uvunaji wa miti Wilayani katika misitu ya asili inayovunwa kwa ajili ya magogo, mbao, nguzo, fito, kuni na mkaa. Mazao hayo ni yale tu yatakayovunwa kwa ajili ya biashara. Jukumu la pili ni kufuatilia utekelezaji wa mpango wa uvunaji katika msitu husika na kutoa ushauri katika ngazi za Wilaya na Wizara pamoja na kufuatilia utekelezaji wa mpango wa upandaji miti katika eneo la msitu unaovunwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.