Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 3 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 33 2021-11-04

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: -

Tanzania ina idadi ya watu takribani milioni hamsini na tano wenye madaraja tofauti ya uchumi: -

Je, katika idadi hiyo Tanzania ina mabilionea wangapi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia utafiti uliofanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kwenye mwaka wa fedha 2014/2015 na baadaye kurejewa mwaka 2019/2020, unaonesha kuwa idadi ya mabilionea duniani inakadiriwa kufikia watu milioni kumi na nne. Kwa mujibu wa Ripoti ya Capgemini and RBC Wealth Management, July 2019. Bara la Afrika pekee lina mabilionea 140,000 sawa na asilimia moja ya mabilionea wote wa dunia nzima. Kati ya idadi ya mabilionea waliopo Barani Afrika, mabilionea 5,740 wanatoka Tanzania ambao wanamiliki asilimia 4.2 ya utajiri katika kundi la mabilionea wa Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha miongoni mwa mabilionea 5,740 waliopo Tanzania, mabilionea 115 sawa na asilimia mbili ya utajiri wa zaidi ya dola milioni 30 wanaomiliki zaidi ya asilimia 28 ya utajiri wote wa mabilionea wanaotoka Tanzania. Kati ya hawa mabilionea waliopo Tanzania wengi wamesajiliwa na Mamlaka ya Mapato yaani TRA na wanalipa kodi zao katika Idara ya Walipa kodi Wakubwa na wamewekeza katika Sekta za Viwanda, Nishati na Madini ikiwemo pia Sekta ya Fedha, Mawasiliano pamoja na Uchukuzi, Utalii na Makazi.