Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 26 2021-11-03

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Wanawake na Watoto wanapata shida Baba wa familia anapofariki; pamoja na Sheria ya Mirathi;

Je Serikali ina mpango gani zaidi wa kumsaidia mjane katika masuala ya mirathi?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyofuatilia na kusemea kwa nguvu kuhusu dhuluma wanazofanyiwa wanawake na watoto mara baada ya baba wa familia kufariki.

Mheshimiwa Spika, sheria zinazohusiana na mirathi, zinatamka wazi kuwa wanufaika wa mirathi ni mke wa marehemu, watoto wa marehemu na wazazi wa marehemu. Vilevile inaelekeza kuwa msimamizi wa mirathi si mrithi wa mali za marehemu labda atokane na makundi tuliyoyataja hapo juu. Uteuzi wa msimamizi wa mirathi hufanywa na kikao cha familia na baadaye kuthibitishwa na Mahakama.

Mheshimiwa Spika, kuendelea kwa vitendo vya dhuluma, udhalilishaji wa familia ya marehemu akiwemo mke na watoto, Serikali imeanza kupitia upya Sheria ya Usimamizi wa Mirathi hiyo katika kubaini mapungufu ili iweze kurekebishwa. Kwa kuwa mchakato huo uhusisha taasisi za dini, mchakato umeanza wa kukutana nao na pia kukutana na viongozi wa makabila mbalimbali ili kupitia mila zao ambazo nyingi ni za udhalilishaji.

Mheshimiwa Spika, ikibainika kutokea vitendo vya dhuluma kwa wanafamilia waliopoteza baba wa familia inaelekezwa kwenda Mahakamani kutafuta haki zao. Nitoe wito kwa Waheshimiwa Wabunge kutoa ushirikiano wa familia hizo ambazo nyingi hazina uelewa mkubwa wa masuala ya kisheria kufikia ili huduma hii na waweze kupata haki zao. Ahsante.