Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 25 2021-11-03

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Kiwanda cha Viuadudu cha Kibaha kinazalisha bio-larvicides za kuangamiza viluilui vya mbu kama ilivyokusudiwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sylvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kiwanda cha viuadudu Kibaha, Tanzania Biotech Products Limited ni mali ya Serikali kwa asilimia 100. Kiwanda hiki kinao uwezo wa kuzalisha lita milioni sita za viuadudu vya kibaolojia (bio-larvicides) kwa mwaka vinavyotumika kuua viluilui wa mbu waenezao Malaria na aina nyinginezo.

Mheshimiwa Spika, kiwanda kinaendelea kuzalisha viuadudu vya kibaolojia ambapo tangu kiwanda kilipoanza uzalishaji mwaka 2017 hadi mwezi Agosti, 2021 kimeweza kuzalisha jumla ya lita 700,286.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali kupitia Shirika letu la Maendeleo ya Taifa (NDC) ni kuhakikisha kiwanda hiki kinazalisha kwa ukamilifu wake (full installed capacity) kwa kutafuta masoko zaidi ya viuadudu ya ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.