Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 24 2021-11-03

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha usikivu wa Radio ya Taifa (TBC) katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Zanzibar?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Othman Hija, Mbunge wa Tumbatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiboresha usikivu wa TBC kwa kutenga fedha katika bajeti ya maendeleo kila mwaka ili kuyafikia maeneo yasiyo na usikivu wa TBC kwa nchi nzima yakiwemo maeneo ya Zanzibar. Miradi iliyotekelezwa na TBC ni pamoja na kufunga mitambo ya kurushia matangazo ya redio katika Visiwa vya Unguja na Pemba.

Mheshimiwa Spika, aidha, miradi ya upanuzi wa usikivu wa TBC inaendelea kutekelezwa katika Mikoa mipya ya Songwe, Njombe na Simiyu. Vilevile upanuzi huo unaendelea kwa upande wa Visiwa vya Unguja na Pemba. Miradi hiyo inatarajiwa kukamilika ifikapo Machi, 2022.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuiwezesha TBC ili maeneo yote nchini ambayo hayana usikivu yakamilike ifikapo mwaka 2025 kama ilivyoainishwa katika Ilani ya uchaguzi ya CCM (2020 – 2025) Ibara ya 125 (f). Ahsante. (Makofi)