Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 13 2021-11-02

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: -

Je Serikali ina mpango gani wa kuyatumia majengo yaliyoachwa na Kampuni ya Ujenzi ya China yaliyopo Kijiji cha Maneme yatumike kama Chuo cha Ufundi (VETA)?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Ally Yahaya Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inayo azma ya kujenga Chuo cha Ufundi Stadi katika Wilaya zote hapa nchini. Kwa sasa Serikali inaendelea na ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi katika Wilaya 29 ambavyo vipo katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa majengo yaliyoachwa na mkandarasi aliyejenga barabara yapo na Wilaya imeona umuhimu wa kuyatumia, Wizara yangu itatuma wataalam kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) washirikiane na wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu kufanya tathmini ya majengo hayo iwapo yanakidhi vigezo vya msingi vya kuanzisha mafunzo ya ufundi stadi.

Mheshimiwa Spika, wakati juhudi hizo zikiendelea, nashauri wananchi wa Wilaya ya Nanyumbu kutumia Vyuo vya Ufundi Stadi vya Mtwara, Lindi na Namtumbo ambavyo vipo jirani na Wilaya hiyo.