Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 8 2021-11-02

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza agizo la Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutaka mwananchi aliyevamia ardhi ya Kijiji cha Nyarututu/Kabanga kurejesha ardhi hiyo kwa Serikali ya Kijiji ili itumike kwa faida ya wananchi?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ardhi ya Kijiji cha Nyarututu yenye ukubwa wa ekari 130 ilipangwa na Serikali ya kijiji cha Nyarututu kwa matumizi ya Umma. Hata hivyo, kumekuwa na mgogoro unaoendelea ambapo Bwana Zacharia Kabutelana amefungua kesi dhidi ya viongozi wa kijiji akidai kwamba aliwahi kupewa eneo hilo na Serikali ya Kijiji.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Bwana Zacharia amefungua maombi Baraza la Ardhi na Nyumba katika Shauri Na. 18/2019 ambapo lipo kwenye hatua za kusikilizwa. Kutokana na eneo hilo kuwa na maslahi ya Umma, Mkurugenzi amepeleka maombi Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ili naye awe sehemu ya kesi hiyo na kuwakilishwa na Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya. Afisa Ardhi wa Halmashauri hiyo ameagizwa kufuatilia kwa karibu shauri hili ili kuhakikisha maslahi ya Serikali yanalindwa.