Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 7 2021-11-02

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa Grid ya Taifa katika Mkoa wa Katavi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa njia kuu ya kusafirisha umeme wa Gridi ya Taifa wa msongo wa kilovolti 132 yenye urefu wa kilometa 381 kutoka Tabora hadi Katavi na ujenzi wa vituo vitatu (3) vya kupoza umeme vya msongo wa kilovolti 132/ 33kV Ipole (Sikonge), Inyonga (Mlele) na Mpanda (Mpanda Mjini).

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa majengo ya kudhibiti mfumo wa umeme (Control Building) ya Ipole, Inyonga na Mpanda yamekamilika. Upimaji wa mkuza (wayleave) kwa ajili ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme (Transmission Line) kutoka Tabora hadi Katavi umekamilika. Zoezi la uthamini wa mali za wananchi katika maeneo yanayopitiwa na mradi limekamilika kwa Wilaya za Mlele na Mpanda Mjini na zoezi hilo linaendelea kwa Wilaya za Tabora, Uyui, na Sikonge na litakamilika mwishoni mwa mwezi wa Novemba, 2021. Mradi unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti, 2023.

Mheshimiwa Spika, gharama ya mradi ni shilingi bilioni 64.9 na fedha hizi zote ni fedha za ndani na ujenzi unafanywa na Wataalamu wa Shirika la TANESCO.