Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 2 2021-11-02

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa barabara ya Nyamisati hadi Bungu katika Jimbo la Kibiti?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Bungu – Nyamisati yenye urefu wa kilometa 40.2 ni barabara ya Mkoa inayohudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) iliyopo katika Wilaya ya Kibiti, Mkoa wa Pwani.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha wa 2021/ 2022, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania, imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii. Taratibu za kumpata mshauri elekezi wa kufanya kazi hiyo, ziko katika hatua za mwisho za kusaini mkataba. Baada ya usanifu kukamilika na gharama kujulikana Serikali itatafuta fedha za ujenzi.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikiendelea na maandalizi ya kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania, inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii. Ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka na katika mwaka huu wa fedha wa 2021/2022 jumla ya Shilingi milioni 732.67 zimetengwa. Ahsante.