Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 119 2021-09-10

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza Kodi kwenye Vifaa vya Mchezo ili Sekta ya Michezo iweze kustawi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa David Mwakaposa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/ 2022 Serikali kwa kuona umuhimu wa Sekta ya Michezo nchini, imetoa msahama wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye nyasi bandia kwa viwanja vya mpira vilivyopo kwenye Manispaa na Majiji.

Aidha, Serikali itaendelea kutoa msamaha wa VAT kwenye nyasi bandia kwa viwanja vya mpira vilivyopo kwenye Halmashauri baada ya kuridhishwa na matumizi ya msamaha uliotolewa kwenye Manispaa na Majiji. Aidha, katika kuendeleza Sekta ya michezo nchini Serikali imetoa msamaha wa VAT kwenye huduma za elimu zitolewazo kwenye vituo vya mafunzo ya michezo nchini.