Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 116 2021-09-10

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: -

Serikali imewekeza kiasi cha Shilingi Bilioni 20 kwa ajili ya kutengeneza miundombinu ya ukaguzi wa magari nchini (Destination Inspection).

Je, ni sababu zipi zilisababisha Serikali kubadilisha mfumo huo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lilianza kukagua magari yaliyotumika yanayoingia nchini kuanzia tarehe 01 Machi, 2021 katika Bandari ya Dar-Es-Salaam. Sababu za kusitisha utaratibu uliokuwepo awali (Pre-Shipment Verification of Conformity to Standards – PVOC) ni pamoja na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa mfumo huo na pia, faida tarajiwa baada ya kutekeleza mfumo wa Destination Inspection (DI).

Mheshimiwa Spika, changamoto za PVOC ni pamoja na Mosi; ukosefu wa ufanisi, gharama kubwa za ukaguzi na upimaji. Mawakala kutokutokuwa na ofisi za ukaguzi katika maeneo yote, mawakala kushindwa kufanya ukaguzi inavyostahili, nchi kupoteza fedha za kigeni, upotevu wa ajira kwa Watanzania, nchi kushindwa kujenga uwezo wa miundombinu ya ukaguzi na wataalam wa ukaguzi na ugumu wa kuhudumia Wajasiriamali Wadogo wanaonunua bidhaa nyingi za aina mbalimbali zenye thamani ndogo.

Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, tangu ukaguzi huu uanze hapa nchini mwezi Machi hadi tarehe 25 Agosti, 2021 jumla ya magari 13,968 yamekaguliwa na TBS na kuliingizia Taifa jumla ya Shilingi 4,888,800,000 ikiwa ni tozo za ukaguzi. Aidha, wateja wengi wameridhika na kufurahia utaratibu huu wa DI. Nashukuru.