Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 114 2021-09-10

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaunganisha Wakulima wa Mikoa ya Kusini hususan Mkoa wa Njombe na Wawekezaji wa nje na ndani?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pindi Hazara Chana Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa kuwaunganisha wakulima na wawekezaji wa ndani na nje ili kuwa na mfumo endelevu unaowapa fursa ya wote kuwepo na kwa faida ya pande zote mbili. Katika kutekeleza mpango huo, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imekuwa inaratibu makubaliano kati ya wanunuzi/wasindikaji na wakulima kupitia kilimo cha Mkataba kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa teknolojia, pembejeo pamoja na masoko.

Mheshimiwa Spika, kupitia ushoroba wa maendeleo wa SAGCOT, Wizara imehamasisha wawakezaji Tanzania Agrofood Ltd & Olivado Ltd katika Mikoa ya Njombe na Iringa ambao wameunganishwa na wakulima wadogo na kuwezesha kuongezeka kwa mauzo wa mazao mbalimbali mfano parachichi. Mauzo yameongezeka kutoka tani 3,696 mwaka 2015 hadi tani 7,190 mwaka 2019.

Aidha, bei parachichi pia imeongezeka kutoka shilingi 1,200,000 kwa tani mwaka 2015 hadi shilingi 1,800,000 kwa tani mwaka 2020. Uwepo wa kampuni hizo zinazowahakikishia wakulima soko imekuwa ni chachu ya kuongezeka kwa uzalishaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia program ya Agri-connect inayotekelezwa kwa uratibu wa Wizara ya Kilimo moja ya nguzo zake ni kuunganisha wakulima na wewekezaji katika mnyororo wa thamani. Programu hiyo katika Mikoa ya Kusini ukiwemo Mkoa wa Njombe ambapo mazao ya kipaumbele ni mazao ya bustani, chai na kahawa. Programu hiyo inalenga kuwaunganisha wakulima na masoko ya ndani na ya nje.