Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 113 2021-09-10

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, Serikali imesaidia mikopo kwa vikundi vingapi vya wavuvi Wilaya ya Nkasi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025 Ibara ya 43(h) inaelekeza Serikali ihamasishe uanzishaji na uimarishaji wa vikundi na Vyama vya Ushirika vya Msingi vya Wavuvi wadogo kwa lengo la kuwapatia mitaji, ujuzi na vifaa pamoja na zana za uvuvi. Katika kutekeleza ahadi hiyo, Serikali imefanya yafuatayo: -

(a) Imeendelea kuhamasisha wavuvi kujiunga kwenye Vyama vya Ushirika vya Wavuvi ambapo kwa mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya wadau 16,733 kutoka halmashauri 21 nchini wamepatiwa mafunzo hayo ikiwemo halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ambapo hadi sasa jumla ya Vyama vya Ushirika 146 vya Wavuvi vimeundwa.

(b) Serikali imeendelea kuwezesha wavuvi kupitia Vyama vya Ushirika vya Wavuvi kwa kuvipatia injini za boti, ambapo kwa sasa Serikali ipo kwenye mchakato wa kuvipatia injini za kupachika Vyama vya Ushirika vya Wavuvi kumi kikiwemo Chama cha Ushirika Kabwe kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi, ahsante.