Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 107 2021-09-10

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutimiza masharti ya ajira kwa watumishi ikiwa ni pamoja na kuwapandisha madaraja na stahiki nyingine?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutimiza masharti ya ajira kwa watumishi wake ikiwemo kupandisha vyeo Watumishi, ambapo Serikali ilitoa barua Kumb. Na. BC.46/97/03D/59 ya tarehe 28 Aprili, 2021 iliyoruhusu upandishwaji vyeo kwa Watumishi wa Umma kuanzia tarehe 1 Juni, 2021. Hadi kufikia tarehe 1 Septemba, 2021, jumla ya Watumishi wa Umma 174,222 wamepandishwa vyeo na kubadilishiwa mishahara yao.

Aidha, Serikali itaendelea kuboresha maslahi kwa watumishi wa umma kadri bajeti itakavyoruhusu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.