Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 105 2021-09-10

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, ni lini Vituo vya Afya vya Mapera na Muungano vitaanza kutoa huduma ya upasuaji ambao haufanyiki kutokana na kukosekana kwa baadhi ya vifaa ikiwemo sterilizer?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali katika Mwaka wa Fedha 2019/2020 iliipatia Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga shilingi milioni 400 kwa ajilii ya ukarabati na upanuzi wa Kituo cha Afya Mapera ambapo ujenzi umekamilika na kituo hicho kimeanza kutoa huduma kuanzia Julai, 2021. Mpaka sasa akinamama wajawazito 11 wamekwishanufaika na huduma ya upasuaji.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Muungano kilianza kujengwa mwaka 2017 kwa nguvu za wananchi na fedha za mapato ya ndani ya halmashauri. Katika Mwaka wa Fedha 2019/2020 Serikali ilitoa shilingi milioni 60 ili kuendeleza ujenzi wa kituo hicho. Jengo la wagonjwa wa nje (OPD) limekamilika na limeanza kutoa huduma kuanzia Julai, 2021. Ujenzi wa jengo la upasuaji unaendelea na upo kwenye hatua ya ukamilishaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kujenga na kukarabati vituo vya afya nchini ikiwemo Vituo vya Afya vya Mapera na Muungano ili kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya, dawa na vifaa tiba kote nchini.