Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 100 2021-09-09

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu usalama wa Askari ambao wakati mwingine huvamiwa na kujeruhiwa pamoja na kuporwa silaha wakati wakiwa kazini?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge Viti Maalum kutoka Zanzibar, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Askari wa Jeshi la Polisi wapo imara katika kutimiza majukumu ya kazi zao za kila siku na wamepata mafunzo mbalimbali yakiwemo mafunzo ya mbinu za medani, matumizi ya silaha na mafunzo ya kujihami. Pia katika utendaji wa kazi wao hufuata utaratibu wa kujilinda na kulinda wengine, ila mazingira na maeneo ya utendaji kazi husababisha changamoto mbalimbali kutokea kama hizo za kuvamiwa na kujeruhiwa. Mara zote Jeshi la Polisi hudhibiti hali hiyo na kushughulikia kwa haraka matukio ya namna hiyo na kuimarisha amani na utulivu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.