Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 99 2021-09-09

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kutenga fedha za kuvunja Mlima Londo ili kuunganisha Wilaya ya Malinyi na Namtumbo hata kwa kiwango cha changarawe ili njia hii iweze kupitika huku Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa –Kwa Mpepo – Namtumbo Lumecha ya kilomita 296?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatayo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ilikamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Ifakara – Lupiro –Malinyi – Kilosa Kwa Mpepo – Londo – Lumecha mwaka 2018. Katika usanifu huo, barabara itakayojengwa imeukwepa Mlima Londo kutokana na gharama kubwa ya kuuvunja mlima itakapopita barabara hiyo. Hivyo, Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kupita katika maeneo yaliyoainishwa katika upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, namsihi Mheshimiwa Mbunge awe na subira wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Aidha, Serikali itaendelea kuifanyia matengenezo barabara hii na kuendelea kuifungua kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.