Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 98 2021-09-09

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhuisha vigezo vya mfumo wa miradi ya kimkakati kupitia maandiko ya miradi ili iweze kusaidia Halmashauri kubuni miradi ya kiuchumi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imejikita katika kutoa huduma bora na zenye uhakika kwa wananchi wake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba Mamlaka za Serikali za Mitaa zinaendelea kujiongezea mapato kwa kutumia fursa zilizopo katika maeneo yao ili kutoa huduma bora kwa lengo la kupunguza utegemezi wa ruzuku kutoka Serikali Kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kufikia lengo hili, Serikali iliandaa mkakati maalum wa kuwezesha halmashauri kujitegemea kimapato. Katika kutekeleza mkakati huo, Mamlaka za Serikali za Mitaa zinatakiwa kuhakikisha zinatumia kwa ukamilifu fursa za kimapato zilizopo katika maeneo yao na kuongeza uwezo wa kujitegemea kimapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha za kugharamia miradi ya kimkakati hutolewa kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa na Wizara ya Fedha Mipango. Hivyo, hoja ya Mheshimiwa Mbunge kuhusu uboreshaji wa vigezo vilivyowekwa kwenye uchambuzi wa miradi ya kimkakati imechukuliwa na kwa sasa Serikali inaangalia njia bora itakayosaidia kuboresha utaratibu wa maombi na vigezo vya uandaaji wa miradi ya kimkakati kabla ya utoaji wa fedha.