Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 52 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 451 2016-06-28

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. HAFIDH ALI TAHIR (K.n.y. MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN) aliuliza:-
Suala la raia kupigwa na kuharibiwa mali zao kwa upande wa Zanzibar limekuwa likiongezeka siku hadi siku;
Je, Serikali inatambua tatizo hili na kama inatambua inachukua hatua gani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yussuf Salim Hussein, Mbunge wa Chambani kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua kwamba kila inapofika wakati wa Uchaguzi Mkuu hasa katika kisiwa cha Pemba baadhi ya watu hujichukulia sheria mkononi kwa kuwapiga wengine na kuharibu mali zao. Aidha, Serikali itaendelea kuongeza vikosi vya ulinzi na usalama katika maeneo yote tete na kuhakikisha utii wa sheria bila shuruti unazingatiwa. Pia Serikali itaendelea kuelimisha wananchi madhara ya kujichukulia sheria mkononi dhidi ya wengine wasio na hatia.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupitia Bunge lako Tukufu nitoe wito kwa wananchi wote kuacha mihemko na itikadi za kisiasa wakati na kabla ya uchaguzi kwani hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.