Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 94 2021-09-08

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: -

Je, ni lini wananchi wa Kata Saba za Tarafa ya Chamriho watapatiwa maji kutoka mradi wa maji ya Ziwa Victoria?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ni endelevu. Kwa kata saba zilizopo Tarafa ya Chamriho, upatikanaji wa huduma ya maji ni asilimia 61, ambapo vijiji vyote katika Kata tatu za Hunyari, Salama na Nyamuswa vinapata maji kutoka kwenye visima na chemchem.

Mheshimiwa Naibu Spika, na Kata nne, vijiji ambavyo huduma ya maji siyo ya uhakika ni Mahanga na Mamicheru katika Kata ya Mihingo, Kiroeli, Kambumbu na Nyambuzume Kata ya Nyamanguta, Marambeka na Nyamburumbu Kata ya Ketere na kijiji cha Sanzate Kata ya Mgeta.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 mpango wa muda mfupi ni kuboresha huduma ya maji katika vijiji hivyo sita, kupitia utekelezaji wa miradi wa visima virefu ambao utaanza mwezi Oktoba, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkakati wa Serikali ni kutumia vyanzo vya maji vya uhakika hasa Maziwa makuu. Hivyo, mpango wa muda mrefu ni kufanya upanuzi kutoka miradi mikubwa ya maji inayotumia maji ya Ziwa Victoria.