Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 92 2021-09-08

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italeta Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa Bungeni ili kurekebisha Vifungu vya Sheria vinavyohusu Mtoto wa Kike kuolewa akiwa na umri chini ya miaka 18?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zainab Athuman Katimba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali wa yote, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi za ufuatiliaji kuhusu marekebisho ya Sheria ya Ndoa na kutaka kujua ni lini Muswada huu utawasilishwa Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, ikumbukwe kuwa Muswada wa Sheria ya Ndoa ulifikishwa kwenye Kamati ya Katiba na Sheria mwezi Februari, 2021 kufuatia maamuzi ya Mahakama ya Rufani katika Kesi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi Rebecca Gyumi, Rufaa Na. 204 ya 2017 na Na.5 ya 2016 ya Mahakama Kuu iliyotaka Sheria ya Ndoa ifanyiwe marekebisho ili mtoto wa kike aolewe akiwa na miaka 18. Kamati baada ya mapitio iliona upo uhitaji wa ushirikishwaji wa wadau wengi zaidi ili kupata maoni zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na zoezi la kushirikisha wadau ambapo hadi sasa Serikali imeweza kufanya mikutano na Viongozi wa Dini katika Mkoa wa Dar es Salaam mwezi Machi, 2021.

Mheshimiwa NaibU Spika, mMkutano wa pili ulifanyika Jijini Dodoma tarehe 2 Julai, 2021 uliojumuisha Wabunge wa Mkoa wa Dodoma na Viongozi wa Halmashauri ya Mkoa wa Dodoma. Kurejeshwa kwa Muswada huu Serikalini kulitokana na unyeti wa jambo lenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumwarifu Mheshimiwa Mbunge kuwa, Serikali itakapokamilisha michakato iliyoelekezwa na Kamati ya Bunge lako Tukufu, Muswada huu utawasilishwa kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kisha kuwasilishwa mbele ya Bunge lako Tukufu kwa ajili ya Kutunga Sheria husika. Ahsante.