Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 90 2021-09-08

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: -

(a) Je, ni lini Jimbo la Sengerema litapata Kivuko kipya angalau kimoja kati ya vivuko vitano ambavyo Serikali imepanga kujenga katika Ziwa Victoria kwa bajeti ya mwaka 2021-2022?

(b) Je, Serikali inafahamu adha ya usafiri wanayoipata wananchi wa Mji Mdogo wa Buyagu Wilayani Sengerema pamoja na wananchi wa Wilaya za Misungwi na Nyang’hwale kwa kukosa chombo madhubuti cha usafiri wa majini?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

MHE. NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tabasam Hamisi Mwagao, Mbunge wa Sengerema, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo: -

(a) Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imepanga kufanya upembuzi yakinifu ili kubaini aina na ukubwa wa kivuko kinachohitajika katika eneo hilo. Mara baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu na gharama za kivuko hicho kujulikana, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kivuko kipya katika Jimbo la Sengerema kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imepokea changamoto ya adha ya usafiri iliyowasilishwa na Mheshimiwa Mbunge. Wizara yangu katika mwaka wa fedha 2021/2022 itatumia wataalam kufanya upembuzi yakinifu katika eneo la Buyagu Wilaya ya Sengerema na Nyang’wale Wilaya ya Misungwi. Upembuzi yakinifu huo utasaidia kubaini aina na ukubwa wa kivuko kinachofaa ili kiwekwe kwenye mpango wa utekelezaji katika mwaka wa fedha 2022/2023. Ahsante.