Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 87 2021-09-08

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafanya tathmini ya mashamba pori yasiyoendelezwa Mkoani Morogoro?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwezi Julai 2020 hadi Julai 2021, jumla ya mashamba 160 yamekaguliwa katika Mkoa wa Morogoro. Kati ya mashamba hayo, mashamba 123 yapo Kilosa, Kilombero (3), Mvomero (13) na Morogoro (21). Aidha, mwezi Aprili, 2021 Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Sita, Samia Suluhu Hassan, amebatilisha umiliki wa mashamba 11 yenye ekari 24,159 kutokana na wamiliki wake kukiuka masharti ya umiliki.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inafanya utaratibu wa kuyapanga na kuyapima kwa ajili ya matumizi ya wananchi, uwekezaji na ardhi ya akiba na hivi sasa wataalam wanaofanya kazi hiyo wako kwenye maeneo hayo. Kwa sasa Serikali inaendelea na ukaguzi wa mashamba mengine katika Wilaya za Morogoro, mashamba 44 na Mvomero, mashamba 86. Baada ya ukaguzi huo hatua za kisheria zitafuata kwa wamiliki watakaokiuka masharti ya umiliki.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kulifahamisha Bunge lako Tukufu kuwa ukaguzi na uhakiki wa mashamba katika Mkoa wa Morogoro ni zoezi endelevu likiwa na maslahi mapana ya Taifa ya kuhakikisha kuwa tunaondoa migogoro inayojitokeza kwa kuwepo mashamba yasiyoendelezwa ipasavyo.