Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 82 2021-09-08

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka na wa kudumu wa kudhibiti wanyamapori katika Hifadhi ya Taifa Serengeti hasa Tembo na Simba ambao wamekuwa wakivamia vijiji na kuharibu mashamba pamoja na kuua watu?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI K. n. y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jeremiah Mrimi Amsabi, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mwingiliano kati ya binadamu na wanyamapori umekuwepo kwa muda mrefu. Hata hivyo, miaka ya hivi karibuni mwingiliano huo umeongezeka na kusababisha madhara kwa wananchi, ikiwa ni pamoja na kuua mifugo na kuharibu mali nyingine za wananchi ikiwemo mazao. Changamoto hii ipo katika maeneo mengi nchini hususan yanayopakana na maeneo yaliyohifadhiwa kama ilivyo kwa Hifadhi ya Taifa Serengeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia kuwepo kwa changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu katika maeneo mbalimbali nchini, Serikali imeanza kutekeleza Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Kukabiliana na Wanyamapori Wakali na Waharibifu. Mpango huo unahusisha yafuatayo: -

i. Kutoa mafunzo yatakayowawezesha wanajamii kukabiliana na kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu;

ii. Kutoa vifaa mbalimbali kwa ajili ya kujikinga na wanyamapori hao, na wananchi kuhamasishwa kufuga nyuki kwa kutumia mizinga ya kisasa; na

iii. Kutoa namba maalum za simu (toll free number) endapo matukio hayo yanajitokeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.