Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 6 Health and Social Welfare Wizari wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto 77 2021-09-07

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: -

Je, ni kwa kiasi gani suala la kuwapatia wazee wasiojiweza vitambulisho kwa ajili ya kupata matibabu bure limetekelezwa kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Anastazia James Wambura, Mbunge, kwa swali lake zuri na kwa mapenzi yake kwa wazee wetu ambapo nasi ni wazee watarajiwa; kwamba wanaendeleaje hawa wazee wasiojiweza kupata vitambulisho vya kupata matibabu bure, limetekelezwaje.

Mheshimiwa Spika, naomba kulijibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, zoezi la kuwatambua wazee na kuwapatia vitambulisho linaendeshwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa zote hapa nchini. Hadi kufikia Desemba, 2020 jumla ya wazee 2,344,747 wametambuliwa sawa na asilimia 87 ya makadirio ya wazee wote nchini. Kati yao wanaume ni 1,092,310 na wanawake ni 1,252,437. Aidha, wazee wasio na uwezo 1,087,008 wamepatiwa vitambulisho vya matibabu bure na wazee 856,052 wamepatiwa kadi za matibabu za Mfuko wa Afya ya Jamii iliyoboreshwa (iCHF).

Mheshimiwa Spika, vilevile, katika kuhakikisha kuwa makundi yote ikiwemo wazee wanapata huduma bila kuwa na kikwazo cha ugharamiaji, Serikali ipo kwenye hatua ya kuandaa Muswada wa Bima kwa wote utakaowasilishwa kwenye Bunge lako Tukufu ili kuundiwa sheria. Tunatarajia kwa hapa tulipofikia ni Novemba. Ahsante.