Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 6 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 75 2021-09-07

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuleta Sera ya Ubunifu (Innovation Policy) ili kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jidith Salvio Kapinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mchango wa ubunifu na teknolojia kama nyenzo muhimu katika kurahisisha maisha yetu kwa kuokoa muda katika utendaji kazi, kuongeza tija na ubora katika uzalishaji wa bidhaa na hata utoaji huduma.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa ubunifu, mwaka 2012 hadi 2014 Serikali ilifanya mapitio ya Mfumo wa Ubunifu nchini ili kuutambua na kuainisha upungufu uliopo. Mapitio hayo yalitoa mapendekezo ya namna ya kuboresha mfumo huo ili kuleta tija katika shughuli za kijamii na kiuchumi. Aidha, moja ya mapendekezo hayo ni kuwa na sera yenye kuchochea ukuaji wa ubunifu nchini kwa maendeleo ya nchi.

Mheshimiwa Spika, hatukuwa na Sera maalum ya Ubunifu nchini na kwa kuwa, masuala ya ubunifu yanaenda sambamba na sayansi na teknolojia, kwa sasa Serikali inafanya mapitio ya Sera ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia ya mwaka 1996 kwa lengo la kuiboresha ili ijumuishe masuala ya ubunifu. Aidha, maboresho hayo yanalenga kuifanya sera iendane na mabadiliko ya sayansi na teknolojia nchini, kikanda na kimataifa. Hivyo, katika mapitio hayo sehemu ya ubunifu itapewa uzito unaostahili. Ahsante.