Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 62 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 526 2021-06-30

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: -

Hifadhi ya Taifa Mkomazi imebana sana maeneo ya wananchi na kusababisha kazi za kijamii katika Kata za Lunguza, Mng’aro na Mnazi kushindwa kufanyika: -

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kupunguza sehemu ya Hifadhi ya Mkomazi na kugawa kwa Serikali za Vijiji?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Hifadhi ya Taifa Mkomazi imetokana na kupandishwa hadhi kwa lililokuwa Pori la Akiba la Mkomazi kupitia Tangazo la Serikali Namba 27 la mwaka 2008.

Mheshimiwa Naibu Spika, hifadhi hii ni sehemu ya mfumo wa ikolojia wa Tsavo-Mkomazi wenye wanyamapori wengi. Vilevile, ni maeneo ya mtawanyiko na shoroba za wanyamapori na tayari kumekuwa na changamoto nyingi za shughuli za binadamu katika maeneo hayo ambazo zimesababisha kuwepo na migongano kati ya wanyamapori wakali na waharibifu yaani tembo na wananchi wanaozunguka maeneo hayo ya hifadhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, Serikali haina mpango wa kumega eneo hilo kwani kuendelea kumega eneo hilo ni kuendeleza migongano kati ya binadamu na wanyamapori waharibifu kama tembo. Ahsante.