Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 62 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 523 2021-06-30

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Nangurukuru – Liwale yenye kilometa 258 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kama Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 25 inavyoelekeza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa, Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mchakato wa zabuni wa kumpata Mhandisi Mshauri atakayefanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, kwa ajili ya kuijenga Barabara ya Nangurukuru – Liwale yenye urefu wa kilometa 258 kwa kiwango cha lami umeshakamilika na mkataba wa kazi hii unatarajiwa kusainiwa mwishoni mwa mwezi Juni, 2021. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya shilingi milioni
548.603 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo. Kazi ya usanifu itakapokamilika Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.