Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 506 2021-06-28

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: -

Serikali ilikuwa na mpango mzuri juu ya uwepo wa nishati ya gesi asilia nchini, lakini mpaka sasa kumekuwa na sintofahamu juu ya mwendelezo wa uwekezaji wa miradi hiyo ikiwemo gesi ya Mkoa wa Mtwara.

Je, nini kauli ya Serikali juu ya mwendelezo wa miradi hii nchini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shamsia Azizi Mtamba Mbunge wa Mtwara Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) inaendelea na uwekezaji katika sekta ya rasilimali ya gesi nchini kuanzia shughuli za utafutaji, uchorongaji na uendelezaji wa shughuli hizo.

Mheshimiwa Spika, hadi sasa takribani mikataba 11 ya utafutaji na uchimbaji wa gesi asilia inaendelea kufanyiwa kazi kati ya makampuni mbalimbali ya uwekezaji kwa ushirikiano na Serikali kupitia TPDC. Hadi sasa gesi iliyogunduliwa imefikia futi za ujazo trilioni 57.54. Sehemu ya gesi hii hutumika katika kuzalisha umeme kwa asilimia zaidi ya 50 ya umeme wote nchini, lakini pia viwandani, katika majumba na katika magari.

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha kuwa gesi hiyo inaendelea kunufaisha Taifa, Serikali inaendelea kutekeleza mradi mkubwa wa kimkakati wa kuchakata gesi kuwa katika kimiminika (Liquefied Natural Gas – LNG) unaotarajiwa kuanza ujenzi ifikapo mwaka 2023. Serikali kupitia tayari imelipa fidia ya shilingi bilioni 5.71. Gharama ya mradi ni dola za Marekani bilioni 30.5. Mradi unatarajiwa kukamilika ifikapo Juni, 2028.