Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 499 2021-06-28

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: -

Wananchi wa Wilaya ya Same bado wanaendelea kutaabika sana kwa kukosa huduma bora za afya kwenye Hospitali ya Wilaya licha ya ahadi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa ya ujenzi wa hospitali mpya ya Halmashauri ya Wilaya ya Same.

Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa ikizingatiwa kuwa eneo la ujenzi wa hospitali hiyo tayari limeshatengwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Jimbo la Same Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kujenga na kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya nchini zikiwemo Hospitali za Halmashauri. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi bilioni 55.7 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Hospitali 68 za Halmashauri zilizoanza kujengwa katika mwaka wa fedha 2018/2019. Pia Serikali imetenga shilingi bilioni 11.4 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Hospitali 27 za Halmashauri zilizoanza kujengwa katika mwaka wa fedha 2019/2020 na shilingi bilioni 14 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali 28 za Halmashauri katika Halmashauri 28 ambazo hazikuwa na Hospitali za Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa Hospitali kongwe 43 za Halmashauri ambazo zina uchakavu wa miundombinu ikiwemo Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Same. Kupitia Programu ya Ujenzi na Ukarabati wa Vituo vya Kutolea Huduma za Afya nchini; Hospitali hizo zitaanza kujengwa upya kwa awamu kuanzia mwaka wa fedha 2022/ 2023. Ahsante.