Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 57 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 477 2021-06-23

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, Serikali inaweza kuwahakikishia Wananchi wa Moshi Vijijini kuwa barabara za Himo – Kilema, Pofo –Mandaka, Uchira – Kisomachi na Mabogini – Kahe - Chekereni zitawekwa kwenye Bajeti ya mwaka 2021/2022 ambayo pia ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara za Pofo –Mandaka – Kilema, Uchira – Kisomachi – Kolarie, Fongagate – Mabogini – Kahe na Chekereni – Kyomu – Kahe zina jumla ya urefu wa kilometa 57.28. Serikali imeendelea kujenga na kukarabati barabara hizi mwaka hadi mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali ilijenga barabara ya Uchira – Kisomachi -Kolarie kipande chenye urefu wa kilometa 1.4 kwa kiwango cha lami kwa shilingi milioni 694, ujenzi wa barabara ya Chekereni – Kyomu - Kahe kipande cha kilometa 11 kwa kiwango cha changarawe kwa gharama ya shilingi milioni 230.01 na kufanya matengenezo ya barabara za Fongagate – Mabogini - Kahe kipande cha kilometa 3 kwa gharama ya shilingi milioni 60.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mwaka wa Fedha 2020/2021 Serikali inatekeleza kazi za matengenezo ya kawaida katika barabara ya Pofo – Mandaka – Kilema kilometa tisa kwa gharama ya shilingi milioni 13.5, matengenezo ya barabara ya Uchira – Kisomachi – Kolarie kilometa 2.5 kwa gharama ya shilingi milioni 15, matengenezo ya barabara ya Fongagate – Mabogini – Kahe kilometa mbili kwa gharama ya shilingi milioni 60 na matengenezo ya barabara ya Chekereni – Kyomu – Kahe kilomevta 3 kwa gharama ya shilingi milioni 4.5. Matengenezo ya barabara hizi yanaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, Serikali imetenga shilingi milioni 33 kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya Pofo – Mandaka – Kilema kilomita 11, matengenezo ya barabara ya Uchira – Kisomachi – Kolarie kilomita 4 kwa gharama ya shilingi milioni 11 na matengenezo ya barabara ya Fongagate – Mabogini – Kahe kilomita 42.25 kwa gharama ya shilingi milioni 540.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara hizi kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.