Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 55 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 462 2021-06-21

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Bypass ya Mji wa Maswa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mkataba wa kazi ya ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya mchepuo katika mji wa Maswa (Maswa Bypass) yenye urefu wa kilometa 11.3 ulisainiwa tarehe Mosi Juni, 2021 kati ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Kampuni ya M/S CHICO ya China kwa gharama ya shilingi 13,446,688,420.00 na muda wa ujenzi ni miezi 15 ambapo ujenzi wa barabara hii unatarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi Julai, 2021. Ahsante.