Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 55 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 461 2021-06-21

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara ya kutoka Manyoni - Sanza - Chipanga - Bahi hadi Dodoma kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu Swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Manyoni East – Heka - Iseke - Sanza - Chipanga katika Wilaya ya Bahi; Chidilo Juction – Bihawana Juction Dodoma yenye urefu wa kilometa 194 ni barabara ya mkoa inayohudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania TANROADS ambapo ni Mkoa wa Singida na Dodoma. Kati ya hizo kilometa 126 zinasimamiwa na TANROADS Mkoa wa Singida na kilometa 68 ni Mkoa wa Dodoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii kiuchumi, Serikali imeanza na hatua ya kwanza ya ujenzi wa daraja la Sanza ambapo kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa daraja lenye urefu wa mita 75 na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa kilometa 14.5 kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami umekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya Shilingi milioni 1,500, sawa na bilioni 1.5 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Daraja la Sanza ambalo ni kiungo muhimu kwa barabara hii inayounganisha Mkoa wa Singida na Dodoma. Aidha, mipango ya ujenzi wa sehemu ya barabara inayobaki kwa kiwango cha lami itaendelea kufanyika kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.