Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 55 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu 455 2021-06-21

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia watumishi waliostaafu kupata mafao yao kwa wakati?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Costantino Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) ulianzishwa rasmi tarehe 1/ 8/2018 kwa Sheria Namba 2 ya Mwaka 2018. Mfuko huu ni matokeo ya kuunganisha mifuko minne ya awali (LAPF, GEPF, PPF na PSPF) ambayo ilikuwa ikihudumia watumishi mbalimbali wa Umma na kuufanya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kubaki ukihudumia sekta binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati, mipango na utekelezaji wa Serikali katika kuhakikisha watumishi waliostaafu wanapata mafao yao kwa wakati ni kama ifuatayo: -

(i) Kutengeneza mifumo mbalimbali ya TEHAMA ili kuweza kuwatambua wanachama wake na kulipa mafao stahiki pale wanapodai mafao;

(ii) Kulipa malimbikizo mbalimbali ya mafao ya wanachama yaliyopaswa kulipwa na mifuko iliyounganishwa na yale yaliyopokelewa kipindi ambacho mchakato wa kuunganisha mifuko huo ulikuwa unaendelea; na

(iii) Kuandaa ofisi mbalimbali nchini kote na kuweka misingi bora itakayowezesha utoaji wa huduma bora kwa wanachama wake ikiwa ni pamoja na kuimarisha mifumo ya malipo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha wastaafu wanalipwa kwa wakati, waajiri wanakumbushwa kufuata kikamilifu utaratibu ulioainishwa katika Sheria namba 2 ya Mwaka 2018 ambapo inaelekeza ipasavyo maandalizi ya taarifa za wastaafu kabla ya malipo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mifuko imeendelea kuboresha mifumo yake ambapo matarajio ni kuwa waajiri nao wafuate vizuri utaratibu ulioainishwa kisheria ili kupunguza ucheleweshaji wa kulipa mafao kwa wastaafu.