Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 54 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 453 2021-06-18

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: -

(a) Je, ni Vijiji vingapi vya Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya vimepata umeme wa REA II, Densification na REA III?

(b) Je, ni lini vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mbeya Vijijini ina jumla ya vijiji 140. vijiji 101 vina umeme ambao umepatikana kupitia miradi mbalimbali kama ifuatavyo;

REA II Vijiji 21; ujazilizi (Densification) vijiji 24; na mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza vijiji 45. Vijiji 11 vimepatiwa umeme kupitia miradi inayotekelezwa na Shirika la Umeme nchini (TANESCO).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji 39 vilivyobaki ilianza mwezi Mei, 2021 na kazi hiyo, itakamilika ifikapo Disemba, 2022. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 8.05.