Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 54 Water and Irrigation Wizara ya Maji 451 2021-06-18

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza: -

Je, ni lini Tarafa ya Enduimet pamoja na Vijiji vya ELerai, Tingatinga na Sinya vitaunganishwa na mradi wa maji kutoka Mto Simba hadi Longido ambao umepita katika maeneo hayo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Steven Kiruswa, Mbunge wa Jimbo la Longido kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Maji Longido kutoka chanzo cha Maji Mto Simba kulingana na miundombinu iliyopo unazalisha lita 2,160,000. Mradi huo kwa sasa unahudumia Mji wa Longido na Vijiji vya jirani vya Ranchi, Orbomba, Tingatinga pamoja na Mji mdogo wa Namanga na vijiji vya Kimokouwa na Eworendeke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mahitaji ya maji kwa vijiji vya Tingatinga, na Sinya ni zaidi ya lita 500,000 kwa siku, na vinapata huduma ya maji kupitia miradi ya Magadini, Makiwaro na visima virefu vitatu 3 vilivyopo maeneo ya Donyomali, ldonyo na Sinya. Vijiji vingine vya Tarafa ya Enduimet vinapata huduma ya maji kupitia skimu za maji ya Mtiririko ya Tingatinga Ngereyani, Larang’wa na Kamwanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2021/2022, Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya kuboresha huduma ya maji katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Wilaya ya Longido. Aidha, lengo la muda mrefu ni kutumia vyanzo vya uhakika vya maji ikiwemo kufanya upanuzi wa mradi wa kutoa maji Mto Simba hadi Longido.