Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 54 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 448 2021-06-18

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaondoa changamoto ya kukaimu muda mrefu kwa watumishi kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa pamoja na Sekretarieti za Mikoa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua changamoto ya uwepo wa Watumishi wanaokaimu nafasi za uongozi kwa muda mrefu na uchambuzi uliofanyika unaonesha kuwa, watumishi 1,496 wanakaimu nafasi za uongozi katika Taasisi mbalimbali zikiwemo Halmashauri za Wilaya na Sekretarieti za Mikoa. Kati ya hao, watumishi 332 wanakaimu nafasi zao wakiwa na vibali halali kutoka kwa Katibu Mkuu Utumishi na Watumishi 1,164 wanakaimu nafasi zao bila ya kuwa na vibali kutoka kwa Katibu Mkuu Utumishi, Aidha, Kati ya watumishi hawa 1,164 ambao wanakaimu nafasi bila vibali vya Katibu Mkuu Utumishi, jumla ya watumishi 543 hawana ºifa za kukaimu nafasi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa lengo la kutatua changamoto hii, ofisi yangu imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kukusanya taarifa za maafýsa Waandamizi na Wakuu 7,008 katika Utumishi wa Umma wakiwemo watumishi wanaokaimu nafasi hizo ili wafanyiwe upekuzi kwa ajili ya kujaza nafasi wazi za uongozi na zinazokaimiwa kwa muda mrefu.