Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 53 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 446 2021-06-18

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Daraja katika barabara ya Kishanda B limefunikwa na maji, hivyo kukatisha mawasiliano ya Wananchi wa kata za Nyaruzumbura, Nyakatuntu, Kakanja, Kikukuru, Mabila na Kitwe Wilayani Kyerwa.

Je, ni lini Serikali itajenga Daraja katika barabara hiyo ili kuwarejeshea mawasiliano wananchi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALLI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa, Innocent Sebba Bilakwate Mbunge wa Jimbo la Kyerwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kishanda B ni sehemu ya barabara ya Nyaruzumbura –Kishanda yenye jumla ya kilomita 3.4 na eneo korofi kwa maana ya tinga tinga lina urefu wa mita 300. Barabara hii ni muhimu kwa wananchi wa Wilaya ya Kyerwa kwa sababu inaunganisha Makao Makuu ya Wilaya na Kata za Nyaruzumbura, Nyakatuntu, Kikukuru, Mabira na Kitwe katika Wilaya ya Kyerwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na jiografia ya Wilaya ya Kyerwa kuwa na maeneo mengi yenye tinga tinga (swamp areas) Serikali kupitia Mfuko wa Barabara (Road Fund) imekuwa ikitenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya ukarabati wa maeneo korofi ambapo kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka wa fedha 2018/2019 hadi 2020/2021 shilingi milioni 862.54 zimetumika katika maeneo korofi kwa maana ya tinga tinga Wilayani Kyerwa katika barabara za Omukigando-Mkalinzi kilometa 0.18, Isingiro-Ishaka-Ibare kilometa 7.8, Nyabishenge-Nyakakoni kilomita 10, Kamuli- Mtagata-Kigorogoro (Omukagoye swamp) na barabara ya Rwabwere-Karongo kilomita 10 na utekelezaji wa barabara hii unandelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi milioni 33 kwa ajili ya ujenzi wa maboksi kalvati manne ili kusaidia kupitisha maji katika eneo la Kishanda B. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara na madaraja nchini ikiwemo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.