Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 53 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 443 2021-06-17

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, ni lini ukarabati na upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Musoma utakamilika?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther N. Matiko, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha mchakato wa manunuzi kwa ajili ya kumpata mkandarasi atakaetekeleza mradi huu. Aidha, mkataba kati ya Serikali na mkandarasi Beijing Construction Group Co. Ltd umesainiwa Disemba, 2020 na utekelezaji wa mradi huu utakamilika kwa kipindi cha miezi 18, baada ya kuanza hatua za utekelezaji. Hivi sasa Serikali imemaliza awamu ya pili ya malipo ya fidia kwa wananchi watakaopisha mradi huu ili kuruhusu mkandarasi kuanza hatua ya utekelezaji wa ujenzi. Hata hivyo, Serikali imeshamkabidhi mkandarasi eneo la mradi.

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Esther N. Matiko kwamba, Serikali ina nia ya dhati ya kukarabati na kupanua Kiwanja cha Ndege cha Musoma na utekelezaji wake utakamilika baada ya miezi 18 kama nilivyosema nilivyosema. Ahsante.