Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 53 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 442 2021-06-17

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, ni lini Barabara ya kutoka Kibaoni – Kasansa – Muze – Ilemba – Kilyamatundu hadi Mlowo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakangáta, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Kibaoni hadi Mlowo ni barabara ya mkoa yenye jumla ya urefu wa kilomita 363 na inaunganisha mikoa ya Katavi, Rukwa na Songwe. Barabara hii inapita katika bonde la Ziwa Rukwa ambalo ni maarufu kwa uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara pamoja na uvuvi na hivyo kuwa kichocheo kikubwa cha kiuchumi katika mikoa ya Rukwa, Katavi na Songwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, Serikali ilianza mipango ya kuijenga kwa kuanza na ujenzi wa Daraja la Momba ambalo lilikuwa kikwazo kikubwa cha mawasiliano kati ya mikoa hii mitatu ya Rukwa, Katavi na Songwe ambao umekamilika. Ili kukamilisha ujenzi wa barabara yote kwa kiwango cha lami kuanzia Kibaoni hadi Mlowo ambayo ni kilomita 363, Serikali ipo katika hatua ya awali ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambapo kazi inaendelea kwa sehemu ya Kibaoni – Majimoto yenye urefu wa kilomita 27 iliyopo mkoani Katavi na sehemu ya Muze – Kilyamatundu yenye urefu wa kilomita 141 iliyopo Mkoa wa Rukwa. Kwa upande wa Mkoa wa Songwe, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa sehemu ya Mlowo – Kamsamba yenye urefu wa kilomita 130.1 imekamilika na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.