Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 52 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 438 2021-06-16

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaruhusu tena usafirishaji wa vipepeo nje ya nchi ili kuongeza vipato vya wananchi wa Muheza?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamis Mohamed Mwin’juma, Mbunge wa Muheza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo tarehe 17/03/2016, Serikali ilisitisha biashara ya kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi. Tatizo kubwa lililosababisha maamuzi hayo lilikuwa ni ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu za kufanya biashara hiyo, ikiwa ni pamoja na kutokea wimbi kubwa la utoroshaji wa wanyamapori hai. Vilevile Serikali iligundua matokeo hasi yanayoendelea kujitokeza kwa kuendelea kufanya biashara hiyo ikiwemo kuhamisha rasilimali ya wanyamapori nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, Serikali inafanya tathmini ya kina ili kubaini faida na hasara ya usafirishaji wa wanyamapori hai nje ya nchi kwa ajili ya kujiridhisha na biashara hiyo. Baada ya tathmini hiyo Serikali itatoa tamko kwa wadau wa biashara hiyo kuhusu uamuzi uliofikiwa.