Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 429 2021-06-15

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

(a) Je, ni lini wananchi wa Ludewa ambao maeneo yao yamechukuliwa na Serikali kwa muda mrefu kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa Liganga na Mchuchuma watalipwa fidia?

(b) Je, ni lini Mradi wa Liganga na Mchuchuma utaanza kufanya kazi ili kuinua uchumi wa Mkoa wa Njombe na Taifa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Jimbo la Ludewa lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi unganishi wa madini ya chuma na makaa ya mawe ya Liganga na Mchuchuma uliopo katika Wilaya ya Ludewa, Mkoani Njombe ni Mradi wa Kimkakati na upo katika hatua za awali za utekelezaji. Mradi huu unategemea kutekelezwa kwa ubia kati ya Shirika la Maendeleo la Taifa - NDC ambalo litakuwa na 20% na Kampuni ya Sichuan Hongda (Group) Kampuni hii ya China yenye 80% baada ya majadiliano kuhusiana na baadhi ya vipengele katika mkataba wa utekelezaji mradi huu kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ili kuanza utekelezaji wa mradi, mwekezaji aliomba vivutio ambavyo vimeshindwa kutolewa na Serikali kwa sababu vinakinzana na Sheria mpya Na. 6 na 7 za mwaka 2017 ambazo ni Natural Wealth and Resources Contracts (Review and Renegotiation of Unconscionable Terms) Act, 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hadi sasa, majadiliano na mwekezaji huyu yanaendelea ikiwemo suala la ulipaji wa fidia kwa maeneo yote ya mradi yaliyothaminiwa. Utekelezaji wa mradi huo utaanza mara baada ya kukamilika kwa majadiliano hayo.