Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Water and Irrigation Wizara ya Maji 428 2021-06-15

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SEIF K. GULAMALI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Makamu wa Rais ya kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Tarafa ya Simbo na Manonga katika Jimbo la Manonga?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Gulamali, Mbunge wa Manonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa kupeleka maji kutoka Ziwa Victoria, ambapo hadi sasa Vijiji vya Ziba, Igumila, Ibologero, Itibula, Mwalamo, Ngulu, Mwabubele, Nyandekwa, Itale na Usongo vilivyoko katika Tarafa ya Manonga, vimefikiwa na huduma ya maji kupitia mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuanzia mwezi Aprili, 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022, utekelezaji wa miradi ya maji utaendelea endapo mradi wa Maji toka Ziwa Victoria utatekelezwa na utanufaisha vijiji vya Ulaya, Nkinga na Barazani vilivyopo katika Tarafa ya Simbo na vijiji vya Imalilo, Ngulu, Igumila, Ndembezi, Itulashilanga, Njia Panda, Mwanzelwa vilivyopo Tarafa ya Manonga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi zitakazofanyika ni ulazaji wa bomba takribani kilometa 50, kujenga Matenki matano ya kuhifadhia maji katika vijiji vya Igulu (lita 50,000), Ndembezi (lita 100,000), Ulaya (lita 50,000), Kitangili (lita 60,000) na Nkinga (lita 300,000) na kujenga vituo 60 vya kuchotea maji. Utekelezaji wa mradi huu utaboresha hali ya upatikanaji wa maji katika Tarafa ya Simbo na Manonga kufika asilimia 85.